VICHWA MBALIMBALI

MANDELA AOMBEWA AFYA NJEMA KWENYE IBADA YA PASAKA

Makanisa ya Afrika Kusini yamemuombea rais mstaafu Nelson Mandela ambaye anatibiwa homa ya mapafu, pneumonia.


Jumamosi msemaji wa rais, Mac Maharaj, alieleza kuwa Bwana Mandela aliweza kuvuta pumzi bila ya shida na amepata nafuu, lakini bado wasi-wasi ungaliko kuhusu kiongozi huyo wa zamani wa Afrika Kusini mwenye umri wa miaka 94.
Bwana Mandela aliishi mtaa wa Soweto, Johanneburg, kwa miaka mingi.


Mkaazi mmoja wa Soweto, Eddie Vilakazi, aliyemuombea Bwana Mandela katika ibada ya Pasaka Jumapili, anasema anatumai mzee huyo ataishi muda mrefu:
"Mandela ni kiongozi wetu.
Tunamuona kuwa mkombozi wetu.
Ni kila kitu kwetu.
Tunamtakia afya njema haraka.
Mungu amuangalie, ambariki kwa sababu tayari ameshabarikiwa.
Lakini tunamtakia maisha marefu zaidi, awe nasi."

No comments:

Post a Comment

Injili ya Yesu Kristo Designed by INNJILI TANZANIA Copyright © 2013-2015

Injili Tanzania Blog. Theme images by Jason Morrow. Powered by Blogger.